Karibu Ndugu Mtanzania Mzalendo

TAZAMA RAMANI UTALII TANZANIA

Karibu Ndugu Mtanzania Mzalendo

Usiulize Tanzania na Watanzania Watakufanyia nini. Jiulize Wewe Mwenyewe Binafsi Yako Kama Raia Halisia Wa Tanzania Na Mzalendo Halisia wa Taifa Tanzania Utalifanyia Nini Taifa Na Watanzania Ili Siku Ambapo Utakapokufa na Kuiaga Tanzania Na Dunia,  Watanzania Wakumbuke Nyayo au Alama Na Urithi Wako na Kukulilia.

Tazama ramani utalli tanzania marais 6 wa nchii

Tumerithishwa Tuwarithishe

Keeping Tanzania strong & moving Tanzania forward. Proudly and truly Tanzanian.

Karibu Ndugu Mtanzania na Raia wa Taifa letu sote (Mama Tanzania)  Nchi Nzuri na iliyo Mashuhuri Duniani ya Watu Wakarimu na Wastaarabu ya Mlima Kilimanjaro, Visiwa Vya Zanzibari, Pamoja na Tanzanaiti katika Lugha Aushi na Adhimu ya Kiswahili ya Taifa letu Tanzania.  Tuipende, Tuithamini, Tuienzi, Tujivunie na Kuilinda Tanzania kwa Wivu Mkubwa Kwa Ajili Ya Vizazi Vilivyopo Na Vijavyo "Tanzania ni Moja na Hakuna Tanzania B."

VIVUTIO VYA UTALII TANZANIA, KIGANJANI MWAKO NDUGU MTANZANIA MZALENDO

Tazama Ramani

Weka Nafasi Yako ya Safari ya Ndani Sasa!

Jiunge na maelfu ya wazalendo wanaotembelea vivutio vya Tanzania mkoa kwa mkoa. Kupitia Tazama Ramani Utalii Tanzania, weka nafasi yako ya safari kwa urahisi kupitia online booking yetu. Tembelea Serengeti, Ngorongoro, Kilimanjaro, Ziwa Tanganyika na maeneo mengine ya kipekee. Tuipende na tuitetee Tanzania yetu

Mawasiliano Simu ya Mezani:
+255 784 815 517 +255 762 988 420
Barua pepe:
info@domestictourismsafaris.co.tz info@domestictourismsafaris.com
P.O.BOX 17 MOSHI – KILIMANJARO, TANZANIA – EAST AFRICA (N.S.S.F MOSHI COMMERCIAL COMPLEX
Maswali

MASWALI NA MAJIBU YA UFAHAMU ELIMU, UTALI WA NDANI KWA UMMA WA WATANZANIA

MG_0840-scaled.avif

Tunapokea maoni mbalimbali ya wadau wa utalii wa ndani na wanachi kwa ujumla wake katika kujenga na kukuza  sekta hii ya utalii wa ndani.  Kama una ushauri wowote ule wa kujenga nchi yetu sote Tanzania kupitia utalii waweza kuwasilisha maoni hayo kupita barua pepe yetu;  info@tazamaramaniutaliitanzania.co.tz/ info@domestictourismsafaris.com/ info@domestictourismsafaris.co.tz/ edgardowelelo@yahoo.com

 

Je ni pamoja na  Hifadhi za Taifa (National Parks), Mapori ya Akiba ya Wanyamapori (Game Reserves) , Hifadhi za Taifa za Misitu Asilia (National Natural Forests), Mabonde (Valleys), Milima (Mountains), Maeneo ya Kihistoria  Tanzania (Tanzania Historical Sites), Makumbusho ya Taifa Tanzania (Tanzania National Museum), Bustani za Wanyamahai (Animal Zoos), Fukwe za Bahari (Beaches),Maziwa na Mito (Lakes & Rivers), Maporomoko ya Maji (Waterfalls), Miji ya Kihistoria (Historical Towns), Matamasha mbalimbali (Festivals) , Maonyesho (Trade Fairs) ,Riadha (Marathon), Ngoma za Asili (Traditional Dances), na maeneo yenye historia za zama za mawe (Archaeological Sites)  au kwingineko?

Kunapatikana faida nyingi  kwa raia wa Tanzania katika  kuvitembelea na kujionea  vivutio vya utalii;

 

  • i) kujifunza mambo mbalimbali – kunapatikana mambo mbalimbali ya kujifunza kama mtalii wa ndani hususani kwa wanachuo, wanafunzi wa shule za msingi na sekondari,  pia pamoja na wananchi kwa ujumla wake.    

 

  1. ii) Kupumzisha mwili na akili – majukumu ya kila siku ya mwanadamu yamekuwa mengi kiasi cha kufanya watu kushindwa kupata muda wa kupumzika, na mara nyingine kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya digitali watu wamekuwa wakitumia muda wa kupumzika katika matumizi ya simu ambayo pia yanachosha akili. Njia nzuri na bora ya kupumzisha mwili na  akili ni pamoja na  kutoka katika eneo lililozoeleka kwenye ratiba ya kila siku. Iwapo  utapanga muda mara moja wa wiki au mara moja kwa mwezi kutembelea  mojawapo ya vivutio vya utalii utaweza kurudi ukiwa na akili iliyo mpya na kuongeza ufanisi kwenye majukumu ya kila siku. Wengi wamejaribu mbinu hii na kuweza kufanikiwa sana.

 

iii) kujionea maajabu mbalimbali na vitu vipya – Utalii una mabo mengi mapya na mazuri ambayo binadamu anaweza kujifunza na kufurahia.                           

 

  1. iv) Kujaribu vitu ambavyo haujawahi kuvifanya maishani kama kujaribu kuogelea kwenye maziwa na mito. Kujaribu kucheza ngoma za kabila tofauti na la kwako. Kujaribu kufanya matembezi ya miguu ndani ya mapori ya akiba ya wanyamapori, misituni au hifadhi za taifa (National parks).

 

  1. v) Kujenga afya ya mwili na akili hususani ukiwa umetembelea maeneo yanayokutaka kutembea kwa miguu mfano ndani ya hifadhi za taifa (National parks), au katika mapori ya akiba ya wanyamapori (Game reserves).

 

Vi)  Kufurahia na kuburudika uumbaji wa Mwenyezi Mungu – Mwenyezi Mungu ameumba dunia na vitu vyote vilivyoujaza ulimwengu kwa jinsi ya ajabu nay a kushangaza sana. Unapoenda kutalii unapata nafasi ya kuufurahia uumbaji wa Mungu kama vile Maporormoko ya Maji, Mabonde , Mito mikubwa na midogo, Misitu ya asili iliyo ya  aina mbalimbali, pamoja na milima.

Kwa kuwa utalii ni sekta mtambuka: pindi Mtanzania anapotembelea na kujionea vivutio vya utalii  kwa njia moja ama nyingine atahusika moja kwa moja na mambo ya  usafiri, chakula, malazi,  pamoja na ununuzi wa bidhaa mbalimbali hivyo kuwezesha kuongezeka kwa pato la Taifa letu Tanzania, kipato cha mtu mmoja mmoja, ajira kwenye sekta za huduma za utalii pamoja na kusaidia uelewa na ufahamu wa vivutio vya utalii kwa wananchi hivyo kuongeza hali ya uzalendo kwa Watanzania.

Ni pamoja na Hifadhi za Taifa (National parks): Tanzania ina jumla ya Hifadhi za Taifa 21 kwa upande wa Tanzania bara na 1 iliyo pekee visiwani Zanzibar inayofahamika kama ‘’Jozani Chwaka Bay National Park’. Hifadhi za Taifa kwa upande wa Tanzania bara ni pamoja na   Arusha, Tarangire, Ziwa Manyara, Saadani, Mkomazi, Mikumi, Ruaha, Kitulo, Katavi, Udzungwa, Burigi – Chato, Saanane, Nyerere, Gombe, Kisiwa cha Rubondo, Mahale, Ibanda – Kyerwa, Rumanyika – Karagwe, Serengeti,Ugalla,pamoja na  Mlima Kilimanjaro. Hata hivyo,  kusini mwa Tanzania unaweza kutembelea Hifadhi za Taifa ambapo katika kila Hifadhi utakutana na upekee wa aina yake kama vile Maporomoko ya Maji ya Sanje katika Hifadhi ya Taifa ya Milima ya  Udzungwa mkoani Iringa na Morogoro, wanyamapori swala aina ya  kudu wakubwa na kudu wadogo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya  Ruaha mkoani Iringa. Ndege wazuri wenye kupendeza na kuvutia na pia  maua maarufu kama vile  bustani ya Mungu katika Hifadhi ya Taifa ya Kitulo, pamoja na Mabwawa na Mito mizuri ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere  na bila kusahau makundi makubwa ya wanyamapori Nyati au Mbogo katika Hifadhi ya Taifa ya  Mikumi mkoani Morogoro. Viboko, Mamba na Mto mkubwa wa Rufiji  ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere mkoani Pwani, Morogoro, pamoja na Lindi.

Utalii wa ndani kwa wanafunzi au wanachuo  unawezekana. Wanafunzi wote wa shule za Msingi na za Sekondari sanjari na Wanachuo katika vyuo vyao inawezekana kufanya utalii kwa kutembelea maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii nchini kwetu Tanzania kupitia uongozi wao wa shule na chuo kuweza kujipanga na kujiandaa kutalii kupitia waalimu wao. Tovuti hii ya Tazama Ramani Utalii Tanzania (www.tazamaramaniutaliitanzania.co.tz) imekuja kwenu mahsusi ndugu wapendwa watanzania wazalendo katika uelimishaji na uwezeshaji utalii wa ndani kuhusiana na aina mbalimbali za vivutuio vya utalii vinavyopatikana karibia kila kona ya TANZANIA YETU SOTE. Je hauwezi kujitunzia wewe mwenyewe kiasi kidogo cha pesa unayopewa na mzazi/mlezi na kadha wa kadhalika kama mojawapo ya mikakati kutimiza ndoto yako?

Nchi yetu sote ya  Tanzania imejaliwa kuwa na  vivutio  vya aina mbalimbali vikiwemo vivutio vya asili kama vile  mito, mabonde, milima, mapori, Hifadhi za Taifa, na Hifadhi za Misitu; vivutio vya kiutamaduni kama vile vyakula asili, ngoma za asili, mavazi ya asili; vivutio vya kihistoria kama majengo ya kale, na Makumbusho ya Taifa ambapo kumetunzwa historia nyingi za nchi yetu Tanzania.  Tanzania inasemekana kuwa ni  nchi ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii vya asili.

WASHIRIKI WETU

Anza Safari Yako Kupitia Ramani
Tazama Ramani Utalii Tanzania inakuongoza kwenye hifadhi, vivutio, fukwe na maeneo ya utamaduni ukiwa na mwongozo wa njia, umbali, na mawazo ya ratiba ili kupanga safari kwa ujasiri.